jog

jog

Saturday, May 21, 2016

BOSI UNAJISIKIAJE SASA


Kajamaa ambako hakajawahi kusafiri kwa boti kalilazimika kwenda na boti Zanzibar. Kakaa kwenye kiti karibu na dirisha, kabla safari haijaanza, bonge mmoja akaja kukaa pembeni ya kale kajamaa. Safari ikaanza, haukuchukua mda mrefu Bonge akawa anakoroma. Kamjamaa si kakaanza kusikia kichefuchefu, kakawa kanaogopa kumwamsha Bonge ili kapite kakatapike chooni, na kumruka Bonge pia kakawa hakawezi. Kakajitahidi kujikaza lakini bahati mbaya boti ikarushwa na wimbi kakashindwa kujizuia kakaachia tena kakamtapikia Bonge kifuani. Bonge akstuka akaamka akakuta matapishi kwenye shati na suruali yake, wakati Bonge bado anashangaa, Kamjaa kakawahi;
KAMJAMAA: Pole, vipi unajisikiaje sasa?

No comments:

Post a Comment