jog

jog

Thursday, May 26, 2016

KILICHOMFANYA BONGE APUNGUE

Jamaa bonge kaona tangazo
limeandikwa : "Punguza kilo 5 kwa wiki"

Akawapigia simu na kuomba kujiunga, akaambiwa sawa ila awe tayari amefika ofisini saa 12 za
Asubuhi..kesho yake
Siku ya pili akenda na alipofika akapelekwa
kwenye chumba Fulani hivi. Alivyokifungua
akakutana na binti mmoja mzuri kavaa raba,
tight na Tshirt, Binti akasema ukinikamata tuuu
utalala na mimi na binti akaanza kukimbia.
Bonge alimkimbiza yule binti bila mafanikio na
kila siku kazi ikawa hiyo, Yule Bonge akapunguza
kilo 5 ile wiki.
Bonge akaoomba apewe programu ya kupunguza
kilo 10. siku ya pili asubuhi saa 12 alipofungua
mlango akaona bebe ya ukweli ikiwa imevaa
bikini.
Binti kasema ukinishika tuu nakupa mambo
mazuri jamaa na tamaa zake akamkimbiza yule
bebe na mate yanamtoka kila siku kwa wiki ile
mida ilele lakini hakumshika yule mrembo na
akapunguza kilo 10 ndani ya wiki.
Jamaa akanogewa na kuomba programu ya
kupunguza kilo 25
Ofisi akamwuliza kama anauhakika unaitaka hiyo? Kwani ni
programu ngumu sana ...
Jamaa akajibu kwani wanionaje? siwezi shindwa
mimi.
Siku ya pili yake saa kumi na mbili asubuhi
akaenda kufungua chumba kile akitegemea
kukutana na bebe ya ukweli ikiwa tupu, ile
kufungua tuu akakutana na jamaa moja la
miraba minne likimwambia
“ NIKIKUSHIKA TU NAKULA KIBOGA”"
Yule bonge ndani ya ile wiki alipunguza
kilo 40...

Monday, May 23, 2016

KICHEKELESHO CHA LEO:mtoto bhanaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!1

POLISI:We mtoto unauhakika baba na mama yako ndio waliokuibia baiskeli yako??mbona unatuzingua??kwanini wakuibie??
MTOTO:Jamani wala siwadanganyi kwani nina ushahidi kabisaaaaa!
POLISI:Hebu tuambie ushahidi wako!
MTOTO:Jana usiku nilimsikia baba akimwambia mama ikisimama panda kwa juu,nlivyoamka asubuhi nkakuta baiskeli yangu haipo.
POLISI:mhhhhh hili toto boya kweli...

Saturday, May 21, 2016

SORRY NILIKUWA NAKUTANIA


MKAKA: Sweety mambo?
MDADA: Poa asante
MKAKA: Samahani dada, mimi ni kijana ambaye nimekuwa nikikufuatilia kwa muda sasa, na nimegundua wewe ni mtu ambaye ningependa uwe mke wangu niishi nawe milele, naomba nikuoe
MDADA: Haleluya, hatimae sala zangu zimejibu, nimepata taabu sana mimi kaka, nimedanganywa na wanaume wengi nikajitahidi kutumia waganga wengi ili nipate mume haikuwezekana, nikaamua kuokoka , nikafunga sana na kukesha sana na kutoa sadaka sana hakikutokea kitu, nikaamua kujiingiza hata katika klabu za mpira, mwaka mmoja nikawa Yanga mwingine nikawa simba, wapi sikupata mume wa kunioa, nikajikondesha niwe na shepu ya kimiss lakini bure, nikahama toka Moshi nikaenda Tanga na hatimae kuja kuja Dar haikusaidia, nikajiunga na facebook, twitter, instagram, whatsapp nikaanzisha mpaka blog ya kujieleza natafuta mume, sikupata mume  wa kunitamikia atanioa, nikajitahidi kuhudhuria maharusi mbalimbali bure, hatimae leo maombi yangu yamejibu, asante sana kaka niko tayari hata leo kufunga ndoa
MKAKA: Nakutaniaaaaaaaaa

BOSI UNAJISIKIAJE SASA


Kajamaa ambako hakajawahi kusafiri kwa boti kalilazimika kwenda na boti Zanzibar. Kakaa kwenye kiti karibu na dirisha, kabla safari haijaanza, bonge mmoja akaja kukaa pembeni ya kale kajamaa. Safari ikaanza, haukuchukua mda mrefu Bonge akawa anakoroma. Kamjamaa si kakaanza kusikia kichefuchefu, kakawa kanaogopa kumwamsha Bonge ili kapite kakatapike chooni, na kumruka Bonge pia kakawa hakawezi. Kakajitahidi kujikaza lakini bahati mbaya boti ikarushwa na wimbi kakashindwa kujizuia kakaachia tena kakamtapikia Bonge kifuani. Bonge akstuka akaamka akakuta matapishi kwenye shati na suruali yake, wakati Bonge bado anashangaa, Kamjaa kakawahi;
KAMJAMAA: Pole, vipi unajisikiaje sasa?

Sunday, October 5, 2014

KICHEKELEO:HUYU NAE

MGONJWA:Dokta kuna ndoto inanijia kila usiku naomba msaada wako
DOKTA: Unaota nini?
MGONJWA: Dokta naona mademu masupasta wote wa bongo wanapigania kunibaka, me napigana nao nawatandika mangumi mpaka wanakimbia wote
DOKTA: Sasa watakaje ndugu yangu
MGONJWA: Dokta tafadhali nikate hii mikono